
Unyanyasishaji wa Nyumbani na Familia - Baadhi ya watu, pamoja na baadhi ya watu wa Kiaborigini na Kisiwa cha Torres, wanapendelea neno 'unyanyasishaji wa familia' kwa sababu linadeskribu aina mbalimbali za mahusiano ambapo unyanyasishaji unaweza kutokea, na pia kunakiri athari za udhalimu kwenye familia nzima. Watu wengine wanapenda neno 'unyanyasishaji wa nyumbani' kwa sababu linadeskribu dinamiki zinazopatikana maalum katika mahusiano ya dharau baina ya washirika wa karibu. Katika wavuti huu, tunazungumzia unyanyasishaji wa nyumbani na familia.
Ili ujue zaidi, angalia nini kinamaanisha unyanyasishaji wa nyumbani na familia?
Dhadhiu/ Mshindi - Baadhi ya watu ambao wanaendelea na, au walishapitia unyanyasishaji wa nyumbani na familia hutumia neno 'dhadhiu' kujiwasilisha. Wengine wanapinga kuwa 'mshindi' hueleza vizuri zaidi uzoefu wao. Tunatambua kuwa uzoefu wa kila mtu ni wa kipekee na unategemea hali zake. Kwa uthabiti, wakati mwingine tunazungumza kuhusu watu wanaoendelea na, au walishapitia unyanyasishaji wa nyumbani na familia, kama 'dhadhiu'.
Familia/ Mzazi –Tunatambua kuwa kila familia ni tofauti. Mara nyingi mtoto hulindwa na mtu asiye mzazi wake wa asilia. Kwa mfano, babu, shangazi, mjomba, kaka, mzazi usiokuwa wa asilia au mlezi. Kwa uthabiti, tunapozungumzia sheria ya familia, tunazungumza kuhusu 'wazazi' wa mtoto. Taarifa hii inaweza kuwa muhimu pia kwa wazazi wasio wa asilia.
Mahakama za Familia –Sheria ya familia migogoro inaweza kushughulikiwa katika mahakama mbalimbali. Tunapozungumzia migogoro ya sheria ya familia, tunazungumzia 'Mahakama za Familia' ambazo zinajumuisha:
- Mahakama ya Halmashauri ya Kikanda ya Australia
- Mahakama ya Familia ya Australia
- Mahakama ya Familia ya Western Australia
Wakati mwingine, migogoro ya sheria ya familia pia inahusishwa katika Mahakama ya Eneo au ya Wilaya. Angalia, jinsi gani mfumo wa sheria ya familia unafanya kazi?